KISWAHILI MTIHANI WA KWANZA WA UTAMILIFU VII 2010

SEHEMU A: SARUFI




Andika herufi ya jibu sahihi



Urefu wake ulifanya acheze vizuri mpira wa kikapu. Neno urefu limetumika kama

(a) nomino (b) kielezi (c) kivumishi (d) kihisishi (e) kiwakilishi



Juma anacheza mpira. Hii ni kauli ya ________________

(a) kutenda (b) kutendwa (c) kutendewa (d) kitendo (e) kutendana



Katika neno “watasoma” kiambishi kinachoonesha nafsi ni kipi?

(a) –ta - (b) wa - (c) –so- (d) – ma (e) –tas -



“Vidani hivi vimenunuliwa.” Sentensi hii ipo katika wakati gani? _______

(a) desturi (b) uliopita (c) uliopo (d) ujao (e) mtimilifu



Umoja wa sentensi “Kucha zangu zimekatika” ni upi?

(a) Kucha yangu imekatika (b) Ukucha wangu umekatika



(c) Ukucha wako umekatika (d) Kucha imekatika



(e) Kucha zangu imekatika



Kauli taarifa ya sentensi isemayo “Nataka Helena ajibu swali hili upesi” ni ipi? __

(a) Alitaka Helena ajibu swali lile upesi (b) Helena alitaka ajibu swali upesi



(c) Helena alisema namtaka ajibu swali lile (d) Alitaka Helena aulize swali upesi



(d) Helena jibu swali lile upesi



Mariamu angelia kwa sauti _______ msaada.

(a) angelipata (b) angepata (c) angalipata (d) angapata (e) angeripata



Kinyume cha neno ughaibuni ni kipi?

(a) nchi za jirani (b) magharibi (c) nchi za mbali (d) mashariki (e) nchi za nje



Mtoto huyu alikuwa na bidii darasani __________ hakufaulu mtihani.

(a) hivyo (b) hata hivyo (c) angalau (d) aghalabu (e) mintarafu



Hakuna mtu _______ aliyetaka kufahamu masuala hayo.

(a) yoyote (b) wowote (c) yeyote (d) mmoja (e) hata



Neno NGISI lina konsonanti ngapi? ______________

(a) moja (b) mbili (c) tatu (d) nne (e) tano



Kuna irabu ngapi kwenye neno SABASABA? ______________

(a) nne (b) nane (c) nyingi (d) chache (e) moja



Maneno “mrefu, mweusi, mwerevu na mpole” yakitumika pamoja na majina hufanya kazi gani?

(a) kivumishi (b) kielezi (c) kitenzi (d) nomino (e) kiwakilishi



Nyimbo _____ ni nzuri

(a) zetu (b) yetu (c) yao (d) yenu (e) yake



Nomino michezo inatokana na kitenzi ______________

(a) mchezaji (b) chezo (c) cheza (d) kucheza (e) mchezo







SEHEMU B: MISAMIATI



Andika herufi ya jibu sahihi au fuata maelekezo ya swali pasipokuwa na machaguo



Wewe utazungumza kwa ___________ ya mwalimu mkuu

(a) njia (b) niaba (c) mara (d) sababu (e) badala



Nimetuma ujumbe lakini sijapata mrejesho wowote. Neno lililopigiwa mstari lina maana sawa na neno lipi?

(a) asante (b) ushauri (c) mwaliko (d) jibu (e) mawasiliano



Ng’ombe dume aliyehasiwa ambaye hutumika kwa kufanya kazi kama vile kuvuta mkokoteni au kukokota plau huitwa ___________

(a) mbuguma (b) beberu (c) maksai (d) gegedu (e) fahali



Mawaidha ni ______________

(a) wosia (b) maono (c) ushauri (d) maradhi (e) hotuba



Kutembea kwa matao ni kutembea kwa mwendo wa _________

(a) kasuku (b) maringo (c) polepole (d) haraka haraka (e) kuchechemea



Mzee yule ana kibiongo. Kibiongo ni ______________

(a) nundu (b) pua kubwa (c) jicho moja (d) mfupi (e) toinyo



Kinyume cha neno HASIMU ni ___________

(a) adui (b) rafiki (c) ghadhabu (d) aghalabu (e) mzazi



Mtu anayesaliti nchi au serikali huitwa _____________

(a) haini (b) fedhuli (c) mzalendo (d) kaidi (e) fisadi



Wanafunzi wote walipoelezwa walielewa isipokuwa Tino ambaye ni ________

(a) Bilula (b) Renge (c) Damisi (d) Gomesi (e) Luja



Msichana yule ana nywele za __________

(a) singa (b) katani (c) mafuta (d) mnato (e) marashi







SEHEMU C: METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI



Andika herufi ya jibu sahihi au fuata maelekezo ya swali pasipokuwa na machaguo



Kamilisha methali ifuatayo. “Mwacha asili ni ____________

(a) mjinga (b) mtumwa (c) mgeni (d) mtalii (e) mzalendo



Tegua kitendawili kifuatacho. “Kondoo wetu ana ngozi ndani na nyama nje. ____

Dalili ya mvua ni mawingu. Methali nyingine yenye maana sawa na hiyo ni ____

(a) Debe shinda haliachi kutika (b) Mtegemea nundu haachi kunona



(c) Mwanzo wa ngoma ni lele (d) Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni



(e) Mbio za sakafuni huishia ukingoni



Heri kufa macho kuliko ______________

(a) kufa mwili (b) kufa moyo (c) kufariki dunia



(d) kufa masikio (e) kufa mdomo



Manahodha wengi chombo huenda mrama. Ni methali gani kati ya hizi zifuatazo inapingana na hii? ___________

(a) Kwenye watu wengi haliharibiki neno (b) Jungu kuu halikosi ukoko



(d) Mchimba kisima huingia mwenyewe (d) wingi si hoja (e) Wengi wape



Tegua kitendawili kifuatacho. Ajihami bila silaha. ____________

Jibu la kitendawili: “Nikimpiga mwanangu nalia mwenyewe” ni ________

Maana ya nahau “kupiga chuku” ni ipi? __________

(a) kutoa maneno machafu (b) kutoa maelezo ya uongo



(c) kuchukia jambo fulani (d) kusema ukweli (e) kutunza siri



Meli ilitia nanga baharini. “Kutia nanga” maana yake ni ____________

(a) kuondoka (b) kuelea (c) kwenda kasi



(d) kusimama (e) kwenda polepole



Samahani ndugu umenitoka. Maana ya neno umenitoka ni ipi? ___________

(a) umeniacha (b) umenikimbia (c) nimekusahau



(d) umenichoka (e) umenifia







SEHEMU D: UFAHAMU



Soma habari ifuatayo kwa makini kisha jibu swali la 36 – 45







Mashitaka yaliyomkuta Mzee Mkenule hayakuwa ya kawaida na yalivuta umati mkubwa wa watu.



Siku ya hukumu ndiyo usiseme hapakuwa hata na sehemu ya kutema mate. Miji yote kadhalika haikuwa na habari nyingine isipokuwa mashtaka yaliyomkabili Mheshimiwa Mzee Mkenule na majaaliwa yake siku hiyo ya hukumu. Hata maduka yaliyo maarufu maeneo ya miji yalikosa washitiri.



Jaji naye siku hiyo alikuwa na muonekano tofauti, wazee wa baraza walikuwa kama wengine. Haikujulikana mara moja kama ni uzito wa shauri lile, wingi wa watu au macho ya watu yalipatwa na ukungu hata wayatazame mambo kinyume cha yalivyo.



Upande wa mawakili, wataalamu wa sheria wanaojua kupingana kwa vifungu vya sheria katika mambo yote, maana kwao hakuna dogo, rangi nyeupe yaweza kuwa nyekundu au njano kuwa nyeusi ili mradi sheria imetumika kuhalalisha mwanasheria anachosimamia. Nao pia hali ilikuwa nyingine siku hiyo. Wote walivalia suti nyeusi kifuani kuking’ara mashati meupe pee, kana kwamba yametoka kiwandani maalumu kwa ajili hiyo.



Baada ya mabishano makubwa ya wanasheria juu ya shauri linalomkabili mzee Mkenule, hatimaye ilikuwa ni zamu ya jaji kutoa hukumu.



Hukumu ilisomwa kwa muda mrefu, yapata masaa matatu. Jaji alianza na usuli wa kesi yenyewe, kisha mwenendo wa kesi. Hatimaye alihitimisha kwa kumuondolea mashtaka ya Uhaini Mheshimiwa Mkenule kosa ambalo kama angepatikana na hatia angetupwa lupango kwa miaka isiyopungua ishirini na kenda.







MASWALI







Mashitaka yaliyomkabili Mzee Mkenule yalihusu __________

(a) ujangili (b) uhaini (c) uheshimiwa (d) uanasheria (e) uwakili



Neno gani limetumika badala ya sentensi “historia ya mashitaka” kwenye habari uliyosoma?

(a) mwenendo (b) mashtaka (c) shauri (d) usuli (e) kenda



Neno “kenda” lina maana sawa na ________

(a) tisa (b) tano (c) kumi (d) ishirini (e) muongo



Mawakili hubishana katika mambo kwa vifungu vya sheria kwa kuwa ________

(a) hawajui sheria (b) ni wabishi (c) ni weledi wa sheria



(d) basi tu (e) wanavaa suti nyeusi



Ni nani alikuwa akikabiliwa na mashtaka?

(a) Mzee Mkenule (b) Jaji (c) usuli (d) wazee wa baraza (e) wakili



Neno gani limetumika badala ya jela? _______________

Nani alitumia muda mrefu kuzungumza siku ya hukumu? ____________

“Hapakuwa hata na sehemu ya kutema mate.” Maana yake ni _________

(a) usafi wa mazingira (b) wingi wa watu (c) kote kulijaa mate



(d) sehemu yote ni chafu (e) sehemu yote ilikuwa kavu



Kichwa cha habari hii kingefaa kuwa _______________

(a) mashtaka (b) mashtaka ya Mzee Mkenule (c) Hofu



(d) Siku ya Kiyama (e) Kuondolewa mashtaka



Jaji alitoa hukumu baada ya ______________

(a) mabishano ya wanasheria (b) kumuona Mzee Mkenule



(c) Siku ya hukumu (d) wazee wa baraza



(e) Kumuondolea mashtaka Mzee Mkenule







SEHEMU E: UTUNGAJI



Zipange sentensi zifuatazo kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili zilete habari yenye maana







Pale Rais wa nchi yetu alipotangaza kifo cha mpendwa wetu mzee Kawawa.

ilikuwa ni siku ya majonzi kwa watanzania wote.

Mzee huyu ameshawahi kushika nyadhifa mbalimbali nchini mwetu ikiwemo ya uwaziri mkuu.

Kamwe hatutasahau busara na uzalendo aliokuwa nao mzee Kawawa kwa nchi yetu.

Siku ya mwisho kabisa ya mwaka jana …